Mwigulu Nchemba Azua Gumzo Akiapa Bungeni | MASWAYETU BLOG
Breaking News
Loading...

Wednesday, November 18, 2015

Mwigulu Nchemba Azua Gumzo Akiapa Bungeni




Mwigulu Lameck Nchemba Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi akiapa mbele ya Spika Job Ndugai.

Mwigulu Lameck Nchemba Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi amezua gumzo Bungeni katika kikao cha Bunge la 11 kilichoketi leo (Jana) asubuhi wakati Spika wa Bunge Bw.Job Ndugai akiwaapisha wabunge wateule kuwa wabunge rasmi.
Katika zoezi hilo la kuapa ambapo wabunge mbalimbali wamelipitia,kila Mbunge anafika mbele ya Spika na kupewa kitabu chenye maelezo ya kuapia ambapo wabunge asilimia kubwa wamekuwa wakisoma ila ilipofika zamu ya  Nchemba imekuwa tofauti ambapo yeye hakukifungua kitabu chenye maelezo ya kuapia na badala yake kuapa pasipo kusoma kitabuni.
Mara baada ya kumaliza kuapa wabunge walisikika wakimshangilia kwa kumpigia makofi huku baadhi yao wakisema  kuwa  ‘amekariri’.

Mara baada ya kuapa  Nchemba  anakuwa sasa ni mbunge rasmi ambapo anaweza kuanza  kutekeleza majukumu  kama mbunge halali wa jimbo la Iramba Magharibi“Du,amekariri hadi maneno ya kuapia kweli jamaa kiboko” alisikikika akisema mmoja wa wabunge bungeni hapo.

google+

linkedin

MASWAYETU EXCLUSIVE BLOG
  • Karibu katika Mtandao Huu unaotoa Habari Za Uhakika Kutoka Ndani Na Nje Na Tanzania. Kama una Tangazo,Habari,Picha,Ushauri n.k Wasiliana nasi kwa simu namba 0768 260834. Soma Zaidi

    0 comments:

    POST A COMMENT

     

    IDADI YA WASOMAJI